Makocha

Tuna kitu cha kukushangaza. Unaweza fikiria ulikuja kuwa mwalimu wa shule ya jumapili lakini maelezo yako yamebadilika na umekuwa kocha! ndio ni ukweli, mwaka huu tutakuwa tunasoma bibilia na mandhari ya ndondi na tunatarajia kupata raha na michezo. Mwalimu mpendwa. Anza saa hii! kuwa kocha badala ya mwalimu, na itakupa msukumo kujali kwa undani kuhusu kila mwanafunzi kwenye darasa lako, na maendeleo yao wakijitahidi kuwa mabingwa.

Makundi Madogo

Unda makundi madogo ya watoto 3-7. Kila kundi ndogo lahitaji kocha. Makocha hawahitajiki kuhudhuria darasa kila wiki, lakini wanahitajika kuingia darasani na wanafunzi ama wanariadha kila wiki. Mpe jukumu mmoja wa viongozi wakuu kuwa kocha mkuu wa kuongoza na kuwapa motisha makocha wote.

Gawa darasa lako katika makundi madogo madogo ili uwasaidie wanafunzi wako kufanya zoezi wakati wa wiki. Mipango mingi ya shule ya Jumapili imo kanisani, na hazihitaji kazi za nyumbani wakati wa wiki. Hata hivyo, wanafunzi wako hawawezi "ondoa" dhambi katika maisha yao kwa kujifunza kuhusu hilo. Ni lazima waingie katika uwanja na kupambana na dhambi halisi wanayo kumbana nayo wakati wa wiki. Hakika, bila mtu kuwaangalia, hii itakuwa vigumu kufanya. Tafadhali usi "amini neno lao" na kukubali wakati wanafunzi wanasema walifanya zoezi. Ukiwa mzembe katika mpango huu, utakuwa unafundisha wanafunzi wako kukuambia uongo. Hata hivyo, hebu fikiria pamoja nami kwamba kama kweli unaweza funza wanafunzi wako, na kufuatilia kwamba wanafanya kazi za nyumbani, utaona mabadiliko ya kweli katika maisha yao. Katika mwaka wa 1 tu, unaweza kubadilisha maisha yao yote! Wanafunzi wako hawatakuwa wanakariri tunda la Roho Mtakatifu, lakini watakuwa wanajifunza KUISHIA hilo!

Kuwezesha makundi haya madogo, tumetengeneza makaratasi yenye maelezo kwa makocha na kitabu kidogo kwa Kocha wako mkuu. Karatasi hizo za kocha ni za kila mwezi na kila tunda la Roho. Kocha mkuu ana kitabu kidogo kinachoonyesha zoezi kwa jumla kitengo cha miezi 3.

Kijitabu 1 ya Kocha la Mabingwa
Karatasi za Kocha  za 1

Inapatikana tu ukitoa kwenye mtandao (download)

Peana hizi kwa makocha wote kila mwezi. kitengo cha 1: Upendo, Furaha, na Amani

Majukumu ya makocha :

Kocha:

  • Fundisha watoto 3-5.
  • Kutana na wanafunzi kwa dakika 5 kabla na baada ya darasa kila wiki ili kujadili zoezi na kuwatia moyo kuwa mabingwa.
  • Wapigie simu/waandikie ujumbe wanafunzi kila wiki ili kuwakumbusha zoezi. (Mapendekezo = Jumanne)
  • Wapigie simu/waandikie ujumbe wanafunzi mara ya pili ili kupata ripoti ya zoezi lililo fanywa. (Mapendekezo = Ijumaa)
  • Fuatilia zoezi lililo fanywa kwa watoto katika kundi ndogo na kutoa taarifa kwa kocha mkuu kila wiki.

Kocha Mkuu::

  • Kutana na makocha wote kwa muda wa dakika 5 kabla ya darasa kila wiki ili kujadili zoezi na kuwatia moyo wafundishe kwa uaminifu wanafunzi wao.
  • Wapigie simu/waandikie ujumbe makocha kila wiki ili kuwakumbusha zoezi. (Mapendekezo = Jumanne)
  • Wapigie simu/waandikie ujumbe mara ya pili kila wiki ili kupata ripoti ya zoezi lililo fanywa. (Mapendekezo = Ijumaa)
  • Fuatilia zoezi lililo fanywa kwa wanafunzi wote.
  • Fanya mikutano ya mwezi ya kuwainua makocha na familia zao

Kusajilisha

Inaweza kuonekana kama changamoto kwa kusajilisha viongozi zaidi ili uwe na makocha wa kutosha kwa makundi madogo. Hata hivyo, hii haina haja ya kuwa ngumu vile. Hapa kuna baadhi ya mawazo ya kufanya kutafuta makocha iwe RAHISI:

  • Uliza makocha watumike tu kwa mwezi 1. Kila mwezi unashughulikia tunda moja la Roho. Wakati wa kuuliza watu wazima kujitolea, kama utauliza kwa mwezi 1 tu, wengi watakuwa na nia ya kuhusika. Baada ya mwezi wa kwanza, kama utafanya iwe rahisi na kusisimua, watataka kuhusika tena!
  • Ruhusu makocha kuhudhuria kanisa kama kawaida, lakini ufike kanisani dakika 10 mapema ili kukutana na wanafunzi wao. Makocha wako wanaweza hudhuria darasa lako la Jumapili mara moja tu kwa mwezi, na wiki zingine kuhudhuria kanisa kama kawaida na watu wazima
  • Andikia wanafunzi ujumbe badala ya kuwapigia simu. Saidia Makocha wako kupanga kupokea ujumbe moja kwa moja kwa mwezi mzima, ili waweze kwa urahisi kuwasiliana na wanafunzi wao. Usisahau kwamba badala ya kupiga simu kawaida, unaweza pia kutumia akaunti ya Facebook, Twitter, Whatsapp, nk
  • Tenga nafasi katika kanisa kwa makocha kuhifadhi vitu vichache. Ili kuonekana "wachezaji" makocha wako wanaweza vaa kofia za michezo au kuwa na filimbi na chupa za maji. Badala ya kukumbuka kuja na hizi vitu kila juma, waruhusu kuweka katika kanisa. Kwa njia hii makocha wako wanaweza kuvaa nguo zao mara kwa mara kanisani, na kuvutia vitu vichache vya "mchezo" ili kuonekana kama makocha.
  • Tengeneza mkutano wa kila mwezi kwa makocha kujengwa, ili waweze kutaka kuendelea kushiriki katika mpango kama vile mwaka ikiendelea.
  • Tengeneza mkutano za kila mwezi kwa makocha kujengwa, ili waweze kutaka kuendelea kushiriki katika mpango kama vile mwaka ikiendelea.
  • Ruhusu makundi makubwa ikiwezekana. (Kwa msaada wa notisi wa kundi katika Facebook, haiwezi kuwa vigumu kwa mtu kufunza wanafunzi 10).

Mikutano ya kuhamasisha

Kazi kuu ya kocha mkuu ni kuweka makocha motisha. Njia moja muhimu ya kufanya hivyo ni kuandaa mikutano ya kuhamasisha kila mwezi. Unaweza kutoa chakula, kuomba pamoja, kuangalia data za michezo na kuona ni jinsi gani inaweza leta mabadiliko kwa maisha yetu ya Kikristo. Kuongezea, unaweza kutazama wanariadha wa Olimpiki au kutazama sinema za mchezo wa kuhamasisha pamoja mkiwa na popcorn au vyakula vingine vya kutafuna. Jadili na makocha wako wazo kwamba ilikuwa ya thamani kwa wanariadha kufanya kazi kwa bidii, hivyo basi si ni ya thamani hata zaidi kwa ajili yetu kufanya kazi kwa faida ya kiroho na uzima wa milele?

Kijitabu 2 ya Kocha
Kijitabu 2 cha Kocha

Inapatikana tu ukitoa kwenye mtandao (download)

Peana hizi kwa makocha wote kila mwezi. kitengo cha 2: Uvumilivu, Ukarimu na Wema