Watoto ni wa muhimu Kuhusu sisi Mawasiliano Shule ya jumapili Chuo cha bibilia cha likizo YanguWWC:
Tutakuwa tunasoma tunda la Roho. Hata hivyo,sio kuangalia tunda tu bali dhambi zetu nyingi za mwili ambazo hupigana na tunda la Roho. Lengo lako nikusaidia wanafunzi wako kuwa mabingwa. Kufanya hivi, hawafai tu kuelewa mistari ya kukariri na kujifunza hadithi za Biblia, lakini wanahitaji pia kuweka tunda la Roho kwenye vitendo katika maisha yao ya kilasiku.
"Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria. " Wagalatia 5:22-23
Upendo dhidi ya ubinafsi
Hadithi ya Biblia: Yesu afa msalabani
Mathayo 27:27-56
"Katika hili tumelifahamu pendo, kwa kuwa yeye aliutoa uhai wake kwa ajili yetu; imetupasa na sisi kuutoa uhai wetu kwa ajili ya hao ndugu.
"
1 Yona 3:16
Cheza mchezo ambao marafiki wako wanapendekeza,cheza wakati ambao watataka(kama una ruhusa)na ucheze kwa muda wowote mabao wanataka.usiwatajie ule mchezo unataka kucheza.wakati huu,mahitaji yako hayajalishi,kwa sababu unaonyesha mapenzi ya ukweli bila mawazo yoyote kwako.
Upendo dhidi ya mtazamo wa kuhukumu watu
Hadithi ya Biblia: Kibanzi na boriti
Mathayo 7:1-5
“Msihukumu, msije mkahukumiwa ninyi. Kwa kuwa hukumu ile mhukumuyo, ndiyo mtakayohukumiwa; na kipimo kile mpimiacho, ndicho mtakachopimiwa.
"
Mathayo 7:1-2
Ambia mtu “kazi nzuri” na pongezi kwao kwa kitu mzuri ambacho unaona.kuja na kioo ndogo ya mfuko na ushinde nayo siku mzima.wakati unajaribiwa kuhukumu mtu,chukua kioo cha mfuko na ujiangalie.jikumbukushe yakuwa hufai kusaidia wengine kurekebisha makosa yao.
Upendo dhidi ya chuki
Hadithi ya Biblia: Yuda amuuza Yesu
Mathayo 26:14-16
"Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona.
"
1 Yona 4:20
Fanya kitu kizuri kwa mtu ambaye hupendi. Zuia ulimi wakati unaona mtu mwingine akidanganya ama akiwa karibu kufanya kitu kibaya. Usiwaingize kwenye shida.
Upendo dhidi ya kujihalalisha
Hadithi ya Biblia: Mfano wa msamaria mwema
Luka 10:25-37
“Akajibu akasema, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote; na jirani yako kama nafsi yako.”
Luka 10:27
Simama kusaidia mtu ambaye ako na shida,kupuuza visingizio vyote unaweza kuwa nazo vya kutosaidia.fanya kitu maalum kwa mtu ambaye hayuko kwenye kiwango chako cha jamii..
Upendo dhidi ya ubatili wa kiroho
Hadithi ya Biblia: Daudi kuchaguliwa kama mfalme
1 Samuel 16:1-13
"Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya; haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli; huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote. "
1 Wakorintho 13:4-7
Uliza Mungu kama kuna zoezi la kiroho ambalo unafaa kuacha,huku ukielekeza lengo lako kwa UPENDO. Fanya vitendo hii wiki kuonyesha upendo:usiringe,fanya kile ambacho nicha kusaidia wengine,na usiwajibishe watu kwa makosa ambayo wanafanya.
Furaha dhidi ya Wivu
Hadithi ya Biblia: Viongozi wa dini wana wivu
Matendoya mitume 5:12-33
"kwa maana hata sasa ninyi ni watu wa tabia ya mwilini. Maana, ikiwa kwenu kuna husuda na fitina, je! Si watu wa tabia ya mwilini ninyi; tena mnaenenda kwa jinsi ya kibinadamu? "
1 Wakorintho 3:3
Shukuru Mungu kwa vipawa vya kiroho,muonekano wa nje,milki zako,na familia ambayo uko nayo. Uliza Mungu akupe furaha na ridhaa ambayo unayo.chagua mtu ambaye unaweza kuwa unaweza kuwa aliona wivu hapo mbeleni na umpe zawadi ndogo.(usiwaambie kuhusu wivu wako wa kitambo)
Furaha dhidi ya ulafi
Hadithi ya Biblia: Kijana tajiri
Mathayo 19:16-30
“Akawaambia, Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo.”
Luka 12:15
Mpe Mungu baadhi ya pesa yako ya kibinafsi kama sadaka kwa kanisa,bila kujua inaendea nani,tumia baadhi ya pesa yako kutumikia mtu. Kama huna pesa yoyote,chukua unachomiliki naupeane.
Furaha dhidi ya kujihurumia
Hadithi ya Biblia: Yona na mdudu
Yona 4:1-10
"Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi. Mtu asijidanganye mwenyewe; kama mtu akijiona kuwa mwenye hekima miongoni mwenu katika dunia hii, na awe mpumbavu, ili apate kuwa mwenye hekima. "
2 Wakorintho 4:17-18
nyumba ya wasio na makazi, ama huduma ambayo inawapa chakula maskini.njia ingine, tembelea maskini katika hospitali.omba na uulize Mungu akufungue macho katika picha ile kubwa,na akusaidie utoe macho ya kujiangalia mwenyewe.
Furaha dhidi ya kukosa shukrani
Hadithi ya Biblia: Yesu aponya watu kumi wenye ukoma
Luka 17:11-19
"Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru; Nyuani mwake kwa kusifu; Mshukuruni, lihimidini jina lake; "
Zaburi 100:4
Shukuru wazazi wako(ama mtu mwingine)kwa kitu ambacho wao hukupa kila siku.chagua kitu uende bila kwa muda, kama ukumbusho yakuwa huwezi kuwa nacho kila wakati.
Amani dhidi ya Hofu
Hadithi ya Biblia: Eliya alishwa na kunguru
1 Wafalme 17:1-6
"Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa."
Mathayo 6:33
Gawa kitu ambacho unacho na mtu mwingine,atakama inamaanisha itabidi ukae bila. Iwe ni chakula,nguo,nauli ya basi,ama kitu chochote ambacho kitakugharimu pesa. Uliza Mungu atimize mahitaji yako.
Amani dhidi ya woga
Hadithi ya Biblia: Petro atembea juu ya maji
Mathayo 14:22-33
"Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu. [Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]”
Mathayo 17:20-21
Chagua kitu ambacho kinahisi kama haiwezekani,na uweke uwoga kando. Uliza Bwana Yesu akusaidie kufanya. Kisha anza hatua ndani yake.(ni fanikio kwako kwanza, atakama utazama kama vile Petro alizama.kazi nikuchagua kitu ambacho unahisi nikama haiwezekani na kukijaribu)
Amani dhidi ya ugomvi
Hadithi ya Biblia: Geuza shavu hilo lingine
Mathayo 5:38-42
"Kama yamkini, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote.
"
Warumi 12:18
Jiruhusu ufanyiwe kitu kibaya mara moja hii wiki.(uwezekano Zaidi itafanyika yenyewe)kazi yako ya ziada ni kutofanya lolote.
Amani dhidi ya Imani ya kibinafsi
Hadithi ya Biblia: Yesu awapa chakula watu 5000
Luka 9:10-17
"Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu. "
2 Wakorintho 12:9
Uliza Mungu nafasi umtumikie pahali ambapo huna nguvu. Ingia kwenye kanisa na umtumikie huko. Kama umekimya,ongea Zaidi hii wiki. Kama uko na kelele Nyingi,kuwa wa kunyamaza hii wiki.
Uvumilivu dhidi ya kukosa uvumilivu
Hadithi ya Biblia: Ndama ya dhahabu
Kutoka 32
"mkiwezeshwa kwa uwezo wote, kwa kadiri ya nguvu ya utukufu wake, mpate kuwa na saburi ya kila namna na uvumilivu pamoja na furaha" Wakolosai 1:11
Andika kwenye sakafu kile Mungu amekufanyia samani katika siku za nyuma, kisha weka jiwe kama doa la alama. Fanya moja kanisani, kila mwanafunzi akifanya doa lao maalumu, na kufanya lingine nyumbani wakati wa wiki. Baada ya kuweka jiwe doa ya alama yako, shiriki na mtu mwingine kile Mungu alifanya.
Uvumilivu dhidi ya Huzuni
Hadithi ya Biblia: Ayubu anateseka na uvumilivu
Ayubu 1-2
"Hii ndiyo faraja yangu katika
taabu yangu, Ya kwamba ahadi
yako imenihuisha."
Zaburi 119:50
Andika asante kwa Mungu juu ya jambo ambapo uliteseka. Jaribu kusema kama alivyofanya Ayubu, "Bwana alitoa, na Bwana ametwaa. Jina la Bwana lisifiwe.” Shiriki na wengine katika darasa ushuhuda wako kama unaweza.
Uvumilivu dhidi ya Kiburi
Hadithi ya Biblia: Mfalme Nebukadreza
Danieli 4
"Heri mwisho wa neno kuliko mwanzo wake, Na mvumilivu rohoni kuliko mwenye roho ya kiburi." Mhubiri 7:8
Fanya shughuli kadhaa kujinyenyekeza. Unaweza kumpa mtu nafasi yako katika mstari, epuka kutazama kipinda katika runinga ambapo wahusika wamejaa kiburi, peana sehemu yako katika jukwaa au mbele ya wengine, au ruhusu wengine kuwa sahihi.
Uvumilivu dhidi ya Hasira
Hadithi ya Biblia: Daudi, Nabali na Abigaili
1 Samweli 25
"Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka..." Waefeso 4:26
Nunua vitu vichache vidogo upeane kama zawadi. Wakati unapokuwa na hasira, toa bidhaa kwa mtu uliye na hasira naye. Jaribu kupoteza hasira yako kwa kutoa zawadi ndogo kwa watu, na kutazama jinsi uvumilivu wako unavyo kua.
Uvumilivu dhidi ya Haki
Hadithi ya Biblia: Manna na kware
Kutoka 16: 1-18
"Nanyi vumilieni, mthibitishe mioyo yenu, kwa
maana kuja kwake Bwana kunakaribia. Ndugu,
msinung'unikiane, msije mkahukumiwa. Angalieni,
mwamuzi amesimama mbele ya milango."
Yakobo 5: 8-9
Wiki hii hudaiwi na mtu chochote. Kila wakati unataka kuomba kitu, jizuie mwenyewe. Kila wakati unapo jizuia mwenyewe kutoka kuomba chakula, kibali, wakati, au msaada; unapata ushindi dhidi ya dhambi hii.
Wema dhidi ya Kulinganisha
Hadithi ya Biblia: Mfalme Sauli na Daudi
1 Samweli 18: 5-16
"Lakini kila mtu na aipime kazi yake
mwenyewe, ndipo atakapokuwa na sababu
ya kujisifu ndani ya nafsi yake tu, wala si
kwa mwenzake."
Wagalatia 6:4
Jipatie mwenyewe mipira midogo 20 mwanzoni mwa wiki. Kila wakati unapo jipata ukijilinganisha na wengine, ondoa mpira moja. Hii ni pamoja na facebook au vifaa mengine kwenye mtandao ambapo sisi mara nyingi hujilinganisha na wengine. Kama inahitajika, funga facebook kwa wiki nzima.
Wema dhidi ya Udanganyifu
Hadithi ya Biblia: Petro amkana Kristo
Mathayo 26: 31-35, 69-75
"Sikuketi pamoja na watu wa
ubatili, Wala sitaingia mnamo
wanafiki."
Zaburi 26:4
Wiki hii, enda kwa mtu ambaye ulimdanganya, na uwaambie ukweli. Omba msamaha kwa uongo, na uombe wakusamehe. Kila wakati unaporudi na kusema ukweli itakuwa ushindi mwingine mkubwa dhidi ya dhambi hii.
Ukarimu dhidi ya kujiondoa
Hadithi ya Biblia: Ruthu na Naomi
Ruthu 1: 8-22
“Usiwanyimewatu mema yaliyo haki
yao,Ikiwa katika uwezo wa mkono wako
kuyatenda.”
Mithali 3:27
Tafuta mtu wa kumsaidia, hasa kama "sio tatizo lako." Mpe mtu asiye na makao, au labda mtoto katika shule anayehitaji kalamu mpya au Raba. Hakikisha kuwa hawana husiano na wewe, na kwamba huna wajibu au haja ya kuwasaidia.
Ukarimu dhidi ya Uovu Fitina
Hadithi ya Biblia: Esta aokoa watu wake
Esta 3-5
"Ndugu zangu, nimehakikishwa mimi
mwenyewe kwa habari zenu ya kuwa ninyi
nanyi mmejaa wema, mmejazwa elimu yote,
tena mwaweza kuonyana."
Warumi 15:14
Linda mtu wiki hii kutokana na mtu anayewakosea bila sababu. Tunapo linda mtu mwingine, pia tunakabiliana na dhambi hii katika mioyo yetu wenyewe. Hatarisha sifa yako mwenyewe kwa kulinda mtu mwingine.
Wema dhidi ya kutojali
Hadithi ya Biblia: Sodoma na Gomora
Mwanzo 18: 16-33
"Kwake huyo atakaye kuzima roho
inapasa atendewe mema na rafiki;
Hata kwake huyo aachaye kumcha
Mwenyezi."
Ayubu 6:14
Omba na umuulize Mungu ili akuongezee shauku katika moyo wako wiki hii. Tafuta kitu unachoweza kufanya kwa wengine ili uongeze shauku yako kwa wengine. Tembelea huduma fulani na ujifunze kuhusu kile wanachokifanya, saidia katika makazi yanayolisha watu wengine, au tazama video kuhusu mahitaji yalio duniani. Husika mahali uwezavyo.
Uzuri dhidi ya Uovu
Hadithi ya Biblia: Herode na Yohana
Luka 3: 18-20, Mathayo 14: 1-12
"Uache mabaya ukatende mema,
Utafute amani ukaifuatie."
Zaburi 34:14
Tazama karibu nawe uwepo wa uovu, ambapo mtu anaumiza mwingine bila sababu. Tafuta njia ya kuingilia kati wiki hii ili ulinde mtu asiye na hatia. Labda umsaidie atembee njia tofauti kwenda nyumbani kutoka shuleni, mpe chakula cha mchana, au kuwa na kundi la watu 4 wajiunge na wewe katika kutembea pamoja.
Wema dhidi ya Jitihada za Ubinafsi
Hadithi ya Biblia: Mnara wa Babeli
Mwanzo 11: 1-9
"Msitende neno lo lote kwa
kushindana wala kwa majivuno;
bali kwa unyenyekevu, kila mtu na
amhesabu mwenziwe kuwa bora
kuliko nafsi yake."
Wafilipi 2:3
Usifanye lolote wiki hii ili uongeze umaarufu wako au kujulikana. Kila wakati nafasi ikitokea, kataa. Unapofanya hivyo, utakuwa unapiga ngumi dhambi hii jeuri.
Wema Dhidi ya Uchafu
Hadithi ya Biblia: Yusufu na Potifa
Mwanzo 39: 1-21
"Kwa hiyo twawaombea ninyi sikuzote, ili Mungu
wetu awahesabu kuwa mmekustahili kuitwa kwenu,
akatimiza kila haja ya wema na kila kazi ya imani
kwa nguvu"
2 Wathesalonike 1:11
Linda moyo wako wiki hii. Kama kuna kitu umetendewa dhidi yako, kumbuka kwamba wao ndio waliokosa, sio wewe. Sema katika maombi kila siku, "Mimi ni safi mbele yako, Mungu". Kama umefanya kitu dhidi ya mtu mwingine, omba msamaha kwa mtu huyo na pia Mungu. Kisha unaweza kuomba, "Mimi ni msafi mbele yako, Mungu."
Uaminifu dhidi ya Ibada ya sanamu
Hadithi ya Biblia: Sanduku linatekwa
1 Samweli 5: 1-12, 6, 7: 3
"Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala
mfano wa kitu cho chote kilicho juu
mbinguni, wala kilicho chini duniani,
wala kilicho majini chini ya dunia."
Kutoka 20:4
Chagua shughuli ambaye HUWEZI kushiriki katika sababu inaweza kuwa na ibada ya sanamu. Inaweza kuwa ni desturi kuondoa viatu vyako, gwaride ya kutoshiriki katika, mchezo wa kutohudhuria, au kukosa kununua maua wakati wengine wanafanya hivyo.
Uaminifu dhidi ya Uhaini
Hadithi ya Biblia: Shadraka, Meshack na
Abednego
Danieli 3: 1-21
"Ee Bwana, unifundishe njia yako;
Nitakwenda katika kweli yako; Moyo
wangu na ufurahi kulicha jina lako."
Zaburi 86:11
Tafuta nafasi wiki hii kusema waziwazi shuleni au katika jamii kuwa wewe ni Mkristo, na kwamba unaamini Yesu Kristo. Baada ya hapo, furahia kwamba umekuwa mwaminifu na kikundi kidogo, licha ya shinikizo yoyote unakabili.
Uaminifu dhidi ya Kusita
Hadithi ya Biblia: Bwana anamwita Samueli
1 Samweli 3: 1-21
"Basi imani ni kuwa na hakika ya
mambo yatarajiwayo, ni bayana ya
mambo yasiyoonekana."
Waebrania 11:1
Mwombe Mungu azungumze nawe wiki hii, na akuelekeze kufanya kitu fulani. Fanya mazoezi ya kutii mara moja bila kusita. Kama utasahau na kusubiri, uliza Mungu akupe zoezi jingine.
Uaminifu dhidi ya Kutotii
Hadithi ya Biblia: Wapelelezi katika kanaani
Hesabu 13: 1-3,17-33, 14: 1-11
"Musa akawaambia, Kwa nini ninyi
sasa kuyahalifu maagizo ya Bwana?
Maana halitafanikiwa jambo hilo.!"
Hesabu 14:41
Chagua zoezi 2 kutoka kwa Mungu kufanya wiki hii. Ya kwanza iwe ni jambo Mungu alikuuliza USI fanye, na kingine Mungu alikuuliza ufanye. Mtii Mungu katika mambo yote mbili ili kushinda dhidi ya uasi.
Uaminifu dhidi ya kuzuia
Hadithi ya Biblia: Ibrahimu na Isaka
Mwanzo 22: 1-18
"Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza;
kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima
aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa
thawabu wale wamtafutao."
Waebrania 11:6
Je, kuna kitu ambacho Mungu anakuuliza kuachana naye wiki hii? Chukua muda kufi kiria ni nini hio, na kisha kuomba kwamba Mungu akupe nguvu kuachana kwa muda. Inaweza kuwa chai, Facebook, au chakula unaependa. Ili kushinda vita hii, chagua kuachana na jambo hilo wiki mzima.
Uaminifu dhidi ya kutoaminika
Hadithi ya Biblia: Nuhu na Safina
Mwanzo 5:32, 6: 1-22, 7: 1-12
"Lakini mtu atasema, Wewe unayo imani,
nami ninayo matendo. Nionyeshe imani
yako pasipo matendo, nami nitakuonyesha
imani yangu kwa njia ya matendo yangu."
Yakobo 2:18
Chagua eneo la maisha yako ya kuaminika kwa Mungu. Chagua jambo la kufanya kwa Mungu siku moja wiki hii, na kuhakikisha kuaminika ndani yake. Baada ya kumaliza, chagua ahadi nyingine kwa Mungu kwa siku, na kuweka siku gani ya kufanya hivyo. Hakikisha kukamilisha ahadi yako.
Uaminifu dhidi ya Mashaka
Hadithi ya Biblia: Yesu anamtokea Tomaso
Yohana 20: 24-31
"Yesu akamwambia, Wewe, kwa kuwa
umeniona, umesadiki; wa heri wale
wasioona, wakasadiki."
Yohane 20:29
Chagua kuamini Mungu wiki hii juu ya jambo ambalo aliahidi na inaonekana haiwezekani.
Mwambie Mungu kuwa uko tayari kusubiri mpaka tamati ya ahadi. Ili kuonyesha nia yako
ya kusubiri, nenda usimame katika mstari yoyote, kile ambalo huna haja ya kuwa! Andika ni
dakika ngapi ulisubiri katika mstari ili uweze kuripoti kwa kocha yako.
Upole dhidi ya Mgawanyiko
Hadithi ya Biblia: Ibrahimu na Lutu
wagawana
Mwanzo 13: 1-18
"kwa unyenyekevu wote na upole, kwa
uvumilivu, mkichukuliana katika
upendo."
Waefeso 4:2
Ruhusu mtu mwingine kushinda wakati hamkubaliani juu ya jambo fulani. Unaweza chagua kutokubaliana, lakini jizuie mwenyewe kutoka kupambana juu yake. Waruhusu kuwa na maoni yao.
Upole dhidi ya Mila
Hadithi ya Biblia: Safi na chafu
Mathayo 15: 1-20
"Msiwakoseshe Wayahudi wala Wayunani
wala kanisa la Mungu, vile vile kama mimi
niwapendezavyo watu wote katika mambo
yote, nisitake faida yangu mwenyewe, ila
faida yao walio wengi, wapate kuokolewa."
1 Wakorintho 10: 32-33
Chagua wema kwa mtu kuliko mila yako. Hii inamaanisha kuelewa wakati wanavunja mila yako, na bila kutoa maoni kuhusu hilo. Hakikisha usi umize mtu mwingine, au kuchukua tahadhari kwako mwenyewe na zoezi hili.
Upole dhidi ya Uchungu
Hadithi ya Biblia: Caini na Abeli
Mwanzo 4: 1-16
"Uchungu wote na ghadhabu na hasira
na kelele na matukano yaondok
kwenu, pamoja na kila namna ya ubaya."
Waefeso 4:31
Chagua mtu uliye na hasira nao, na uasamehe. Chukua muda katika maombi, na kusema kwa sauti kubwa, "Mimi nimekusamehe."
Kiasi dhidi ya Majaribu
Hadithi ya Biblia: Yesu anajaribiwa
Mathayo 4: 1-11
"Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo
kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu;
ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo;
lakini pamoja na lile jaribu atafanya na
mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili."
1
Wakorintho 10:13
Pinga jaribu moja, na kama unaweza, tumia andiko kama Yesu alivyofanya. Dumisha udhibiti wa tamaa yako, na wala usiruhusu mwenyewe kufungulia jaribu hilo.
Kiasi dhidi ya Kudanganya
Hadithi ya Biblia: Yakobo anaiba Baraka za Esau
Mwanzo 27: 1-36
"limi unenao uongo huwachukia
wale uliowajeruhi; Na kinywa cha
kujipendekeza hutenda uharibifu."
Mithali 26:28
Kila mtu anasema uongo, hata kama wengine tu ni kidogo. Kumbuka hapo nyuma uongo ulisema mwaka huu. Nenda kwa mtu huyo, waambie ukweli, na kuwaambia pole kwa uongo.
Kiasi dhidi ya Uvivu
Hadithi ya Biblia: Wajenzi wenye busara
na wapumbavu
Mathayo 7: 24-27
"Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala
hayatendi, kwake huyo ni dhambi."
Yakobo 4:17
Pambana dhidi ya uvivu yako wiki hii, kwa kuchagua kitu cha kufanya ambaye hutaki kufanya. Hakikisha kukamilisha hayo, na kushirikisha ushuhuda wako na rafi ki.